MANYARA NEWS

Jumanne, 19 Mei 2015

CCM ARUSHA YATOA ONYO KWA WALIOTANGAZA NIA ARUSHA MJINI.

Chama Cha Mapinduzi(CCM) wilayani Arusha kimetoa  onyo kwa wagombea waliojitokeza kutangazania ya kugombea jimbo la Arusha mjini kupiti chama hicho kuacha tabia ya kuchafuana na kuanza kampeni kabla ya muda

Onyo hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na katibu wa chama hicho wilayani Arusha,Ferooz Bano wakati akimkabidhi kanuni za uchaguzi wa CCM mgombea alliyetia nia ya kugombea jimbo la Arusha mjini kupitia chama hicho,Kim Fute

 Mgombea huyo alifika mbele ya ofisi za CCM wilayani hapa kujitambulisha  na kutia nia ambapo mbali na kufanyiwa ukaguzi wa kadi zake za uanachama pia alikabidhiwa kitabu chenye kanuni hizo na kupewa agizo la kutoshiriki kampeni kabla ya muda.

Hadi sasa jumla ya wagombea saba ambao ni Kim Fute,Phillemon Mollel”Monaban”,Mustapha Panju”Bushbuck”,Victor Njau,David Rwenyagira,Deo Mtui,Francis Laiser pamoja na mbunge mstaafu wa jimbo la Arusha mjini,Felix Mrema wamejitokeza kutia nia kuwania jimbo la Arusha mjini.

Akizungumza mara baada kumkabidhi kanuni hizo katibu huyo wa wilaya aliwataka wagombea wote waliojitokeza kutiania kupitia chama hicho kuacha tabia chafu ya kupakana kuandaa sherehe kwa wapiga kura.

 “Muda wa kampeni bado haujafika hatutaki nyinyi wagombea muanzekuchafuana huko mitaani na wala kuandaa vijisherehe”alisema Bano

Hatahivyo,kwa upande wake mgombea huyo mbali na kushukuru mapokezi ofisini hapo pia alihaidi kufuata maagizo ya chama hicho na kusisitiz kwamba atafuata maagizo ya kanuni hizo kwa umakini mkubwa.

Fute,alitangaza rasmi kuinga katika kinyang”anyiro hicho kupitia CCM huku akijitapa kwamba amejipima na kubaini anatosha kuwa mwakilishi wa jimbo la Arusha mjini kwa kuwa amegundua kuna ombwe la uongozi.



Imechapishwa na Arusha Newsroom kwa 05:17
Tuma Hii kwa Barua pepeBlogu Hii!Chapisha kwenye XShiriki kwenye FacebookShiriki kwenye Pinterest

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Chapisho Jipya Taarifa za zamani Nyumbani
Jisajili kwenye: Chapisha Maoni (Atom)

Mwandishi wa habari

Arusha Newsroom
Tazama wasifu wangu kamili

Kumbukumbu la Blogu

  • ►  2014 (1)
    • ►  Oktoba (1)
  • ▼  2015 (83)
    • ▼  Mei (43)
      • Prof Kagwanja Economic with Truth on KDF Pullout C...
      • ZAMZAM WAIBUKA MABINGWA KOMBE LA NG”OMBE JIJINI AR...
      • mfanyabiashara maarufu wa madini kizimbani
      • SERIKALI YARIDHISHWA NA MADINI YALIONDALIWA
      • CORRUPTION TO DECIDE THE 2017 POLL WINNER
      • GDAMS Nairobi 2015: Military Spending Report Relea...
      • CCM ARUSHA YATOA ONYO KWA WALIOTANGAZA NIA ARUSHA ...
      • KARIBU TRAVEL SHOW BRACES TO HOST 8000 VISITORS 16...
      • UAV SECOND ANTI-POACHING TRIAL LAUNCHED IN SELOUS ...
      • MAGAZETI YA HARDNEWS NA BURUDANI JUMANNE MEI19,2015
      • PARTY YA USIKU WA MARAFIKI WA LOWASSA YAFANA ARUSHA
      • MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA BIA...
      • MO AKUTANA NA RAISI WA MSUMBIJI
      • WATIA NIA CCM WAJINADI MBELE YA LOWASSA
      • ELISA MOLLEL ATANGAZA KURUDI TENA ARUMERU MAGHARIBI.
      • BENKI YA NBC YASAIDIA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA
      • MANISPAA YA KINONDONI YAENDELEA KUTEKELEZA AGIZO L...
      • MANISPAA YA KINONDONI KUJENGA MIFEREJI YA KUDUMU
      • NHC Yafungua Rasmi Kituo Cha Huduma Kwa Wateja
      • VIONGOZI WASTAAFU WAJADILIANA KUHUSU AMANI HAPA NC...
      • VIONGOZI WASTAAFU WAJADILIANA KUHUSU AMANI HAPA NC...
      • BALOZI SEIF ATEMBELEA WAATHIRIKA WA MAFURIKO
      • RAISI WA MSUMBIJI AAGA LEO
      • MAGAZETINI LEO BONGO
      • LOWASSA ATIKISA ARUSHA,ACHANGISHA ZAIDI YA SH,MIL ...
      • GOLA YAANZISHA MCHAKATO WA KIONGOZI TUNAYEMTAKA
      • WILDLIFE,HUMAN CO-EXISTENCE IMPRESSES CLINTON FORM...
      • WANA CCM MONDULI WAPINGA KUBURUZWA NA KUPANGIWA NA...
      • MAHAKAMA YA HAKI ZA BINADAMU YA AFRIKA YAWANOA WAA...
      • MAWAZIRI WA AFRIKA YA MASHARIKI (EAC) WAJIFUNGUA K...
      • WANANCHI WALIOTOROKA GHASIA ZA KUMPINGA RAIS NKURU...
      • MWENGE WA UHURU WACHANJA MBUGA VISIWA VYA ZANZIBAR...
      • Mtemvu afanya ziara ya ukaguzi wa maeneo yaliyohar...
      • ANDIKENI WOSIA KUEPUSHA MIGOGORO - WAZIRI MKUU
      • BONDIA FRANSIC CHEKA KUZIPIGA KESHO MAY 30 UKUMBI ...
      • WANAHABARI MKOA WA IRINGA NA POLISI WAKUTANA KATIK...
      • Maadhimisho ya SIKU YA AFRIKA yafanyika Washington DC
      • UMOJA WA WATANZANIA WALIOSOMA NCHINI AUSTRALIA WAZ...
      • WATANZANIA WAMETAKIWA KUONDOKANA NA FIKRA POTOFU J...
      • FAMILIA YA MTOTO ALIYEGONGWA NA GARI NA KUKATWA MI...
      • MITAZAMO HASI KITAMADUNI CHANZO CHA MAUAJI YA WATU...
      • MISHAHARA YA WALIMU KUONGEZWA AGOSTI
      • Waziri wa Kazi na Ajira,Gaudensia Kabaka azindua B...
    • ►  Juni (5)
    • ►  Julai (33)
    • ►  Agosti (2)
Mandhari ya Safiri. Inaendeshwa na Blogger.